Tuesday, August 23, 2016

KUWAUNGANISHA MAAFISA UGANI NA WAKULIMA NI MUHIMU KWA MAENDELEO YA KILIMO


Habari, Tumeanzisha ukurasa unaowaunganisha "Maafisa Ugani" na "Wakulima" ili kuleta elimu ya ugani katika sekta ya kilimo na kufanya kilimo kiwe chenye manufaa. Hii imetokana na changamoto mbalimbali wanazopata wakulima hapa nchini na maeneo ya jirani.

Hivyo sasa kama wewe ni Afisa Ugani unaombwa kujiunga katika kurasa inayoitwa "Farm Extension Link" ambayo inapatikana katika mtandao wa kijamii wa 'facebook'.

Unachotakiwa kufanya, andika neno "Farm Extension Link" katika sehemu ya kutafutia ya facebook kisha kurasa itakuja halafu 'LIKE' utakuwa umeshajiunga.
Tunaanza kuwaleta "Maafisa Ugani" pamoja kisha tutawaomba pia "Wakulima" wajiunge katika ukurasa huu wa "Farm Extension Link" ili kuweza kuelezea changamoto zilizopo katika sekta ya kilimo.
Kama wewe ni "Afisa Ugani" jiunge sasa kama ilivyoelekezwa hapo juu.
Pia fuatilia ukurasa wetu wa "Twitter" kwa kuandika @ExtensionLink utaweza kujiunga.
Shukrani kwa Usikivu wenu.

0 comments:

Post a Comment